Talaka (kutoka Kiarabu طلاق) ni hatua ya ndoa kuvunjika moja kwa moja kabla ya mume au mkekufa.
Ni tofauti na utengano kati yao ambao unatokea au hata unakubaliwa rasmi na mamlaka husika: huo unawezesha au pengine unalenga warudiane baadaye.
Pia ni tofauti na tamko rasmi la mahakama ya nchi au ya dini kwamba ndoa haikufungwa kweli, kutokana na kasoro fulani iliyokuwepo wakati wa arusi.
Vatikani ni nchi pekee ambayo hairuhusu talaka, mbali ya Ufilipino ambayo inairuhusu kwa Waislamu tu.
Desturi na sheria kuhusu hatua hiyo na matokeo yake maishani zinatofautiana sana duniani. Mara nyingi unadaiwa uamuzi wa mamlaka fulani, lakini sehemu nyingine unatosha ule wa mume au wa mke tu au wa wote wawili pamoja. Nchi zilizoendelea kama vile Marekani[1] zina sheria za kudhibiti talaka na mawakili na wanasheria wanaowakilisha wanaotaka talaka.
Kwa kawaida uvunjifu wa ndoa una madhara makubwa kwa wote wawili, hasa yule mwenye hali nyonge zaidi (kwa kawaida mwanamke), lakini kwa namna ya pekee kwa watoto wao ambao wanaweza wakaathirika hasa kisaikolojia.[2]
Singer, Joseph (2005). "Same Sex Marriage, Full Faith and Credit, and the Evasion of Obligation". Pacific Gamble Robinson. 1: 1–51.
Strong, B., DeVault C., & Cohen T. F. (2011). The Marriage and Family Experience: Intimate Relationships in a Changing Society. Belmont, CA: Wadsworth Cengage Learning.
Thomas, S. G. (2011, October 28). The Good Divorce. The New York Times. Retrieved March 15, 2012
Zartler U., Heinz-Martin, V., Arránz Becker, O. (Edts.) (2015): Family Dynamics after Separation. A Life Course Perspective on Post-Divorce Families. Special Issue ZfF, Volume 10, Opladen/Toronto: Barbara Budrich. ISBN 978-3-8474-0686-0.
Makala hii kuhusu mambo ya sheria bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Talaka kama historia yake au uhusiano wake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.